Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Je, Unatambua Sifa za Mungu Zisizoonekana?

Je, Unatambua Sifa za Mungu Zisizoonekana?

Unapoangalia ua lenye rangi nzuri, anga lililojaa nyota, au maporomoko ya maji, je, unaona kazi yenye kustaajabisha ya Muumba? Uumbaji unaotuzunguka unafunua waziwazi sifa zisizoonekana za Yehova. (Ro 1:20) Tukitua na kutafakari kwa makini mambo tunayoona, tunaweza kutambua nguvu za Mungu, upendo wake, hekima, haki, pamoja na ukarimu wake.—Zb 104:24.

Ni zipi baadhi ya kazi za uumbaji wa Yehova unazoona kila siku? Hata ikiwa unaishi jijini, unaweza kuona ndege au miti. Kuchunguza kwa makini uumbaji wa Yehova kunaweza kutusaidia kupunguza mahangaiko, kukazia fikira mambo ya maana zaidi, na kuongeza imani yetu kuhusiana na uwezo wa Yehova wa kututunza milele. (Mt 6:25-32) Ikiwa una watoto, wasaidie watambue sifa zisizo na kifani za Yehova. Kadiri tunavyothamini uumbaji unaotuzunguka, ndivyo tutakavyomkaribia zaidi Muumba.—Zb 8:3, 4.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA MAAJABU YA UUMBAJI YANAFUNUA UTUKUFU WA MUNGU—NURU NA RANGI, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Rangi mbalimbali zinatokezwa kwa njia gani?

  • Ni nini kinachosababisha rangi zinazong’aa zitokee?

  • Kwa nini tunaona rangi mbalimbali angani?

  • Ni rangi zipi zinazovutia za uumbaji ambazo umeona karibu na nyumba yako?

  • Kwa nini tunapaswa kutenga wakati wa kuchunguza kwa makini vitu vya asili?

Nuru na rangi zinafunua nini kuhusu sifa za Yehova?