Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Februari 19-25

ZABURI 8-10

Februari 19-25

Wimbo 2 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. “Nitakusifu, Ee Yehova”!

(Dak. 10)

Yehova ni mwema kwetu kwa njia kubwa sana (Zb 8:​3-6; w21.08 3 ¶6)

Tunafurahi kumsifu Yehova kwa kuwaeleza wengine kuhusu kazi zake zinazostaajabisha (Zb 9:1; w20.05 23 ¶10)

Pia tunamsifu tunapomwimbia kwa moyo wote (Zb 9:2; w22.04 7 ¶13)

JIULIZE, ‘Ninaweza kumsifu Yehova katika njia gani nyingine?’

2. Hazina za Kiroho:

(Dak. 10)

  • Zb 8:3—Mtunga-zaburi alimaanisha nini aliporejelea vidole vya Mungu? (it-1 832)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwenye nyumba anakuambia yeye haamini kuna Mungu. (lmd somo la 5 jambo kuu la 4)

5. Kufuatia Upendezi

(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Katika mazungumzo ya awali, mtu huyu alikuambia haamini kuna Mungu, lakini yuko tayari kuchunguza uthibitisho unaodokeza kwamba kuna Muumba. (th somo la 7)

6. Hotuba

(Dak. 5) w21.06 6-7 ¶15-18—Kichwa: Msaidie Mwanafunzi Wako wa Biblia Amsifu Yehova. (th somo la 10)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 10

7. Jinsi ya Kuzungumza kwa Njia ya Kawaida Unapohubiri Isivyo Rasmi

(Dak. 10) Mazungumzo.

Njia moja ya kuongeza nafasi za kumsifu Yehova ni kwa kuwahubiria wale tunaokutana nao katika shughuli zetu za kila siku. (Zb 35:28) Mwanzoni, huenda tukawa na wasiwasi kuhusu kuhubiri isivyo rasmi. Hata hivyo, tunapojifunza jinsi ya kuanzisha na kuendeleza mazungumzo kwa njia ya kawaida, tunaweza kuwa na matokeo zaidi, na hata tufurahie mahubiri yasiyo rasmi!

Onyesha VIDEO Uwe Tayari Kushiriki “Habari Njema ya Amani”—Chukua Hatua ya Kwanza. Kisha uwaulize wasikilizaji:

Umejifunza nini katika igizo hilo kinachoweza kukusaidia kuwa na matokeo zaidi unapohubiri isivyo rasmi?

Yafuatayo ni madokezo machache yanayoweza kukusaidia kuanzisha mazungumzo:

  •   Uwe macho kutambua nafasi za kuanzisha mazungumzo kila mara unapotoka nyumbani. Sali kuhusu jambo hilo na umwombe Yehova akuongoze kwa watu wenye mioyo minyoofu

  •   Uwe mwenye urafiki na upendezwe kibinafsi na watu unaokutana nao. Jaribu kujifunza jambo fulani kumhusu mtu huyo kinachoweza kukusaidia utambue ni kweli gani za Biblia zitakazomvutia

  •   Ikiwa inafaa, jaribu kuona ikiwa unaweza kupata habari zake za mawasiliano nawe umpe zako

  •   Usivunjike moyo ikiwa mazungumzo yenu yanakwisha kabla ya kumtolea ushahidi

  •   Fikiria kumhusu mtu huyo baada ya mazungumzo yenu. Endelea kumwonyesha upendezi kwa kumtumia kiunganishi cha mstari wa Biblia au makala ya jw.org

Jaribu kufanya hivi: Mtu akikuuliza, ‘Mwisho-juma wako ulikuwaje?,’ mweleze jambo fulani ambalo ulijifunza mkutanoni au kuhusu kazi unayofanya ukiwa mwalimu wa Biblia.

8. Mahitaji ya Kutaniko

(Dak. 5)

9. Funzo la Biblia la Kutaniko

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 65 na Sala