Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Februari 26–Machi 3

ZABURI 11-15

Februari 26–Machi 3

Wimbo 139 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Jiwazie Katika Ulimwengu Mpya wa Mungu Wenye Amani

(Dak. 10)

Jeuri tunayoona leo inatokana na watu kutotii sheria na kutofuata utaratibu uliowekwa (Zb 11:​2, 3; w06 5/15 18 ¶3)

Tunaamini kwamba hivi karibuni Yehova atakomesha jeuri (Zb 11:5; wp16.4 11)

Kutafakari ahadi ya Yehova ya wokovu kunaweza kutusaidia kungojea ukombozi wetu kwa subira (Zb 13:​5, 6; w17.08 6 ¶15)

JARIBU KUFANYA HIVI: Soma Ezekieli 34:​25, na ujiwazie ukiwa katika mazingira yenye amani yanayofafanuliwa hapo.—kr 236 ¶16.

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 14:1—Wakristo wanaweza kuathiriwaje na mtazamo unaofafanuliwa katika andiko hili? (w13 9/15 19 ¶12)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 2) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Mwalike mtu huyo kwenye Ukumbusho. (lmd somo la 5 jambo kuu la 3)

5. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 1) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwalike mtu huyo kwenye Ukumbusho. (lmd somo la 3 jambo kuu la 4)

6. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwenye nyumba anaonyesha upendezi katika mwaliko wa Ukumbusho. (lmd somo la 7 jambo kuu la 4)

7. Kufanya Wanafunzi

(Dak. 5) lff somo la 13 muhtasari, ungejibuje, na lengo. Tumia makala kutoka kwenye sehemu ya “Chunguza Zaidi” ili kumsaidia mwanafunzi wako kuelewa jinsi Mungu anavyohisi kuhusu dini ya uwongo. (th somo la 12)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 8

8. “Hekima Ni Bora Kuliko Silaha za Vita”

(Dak. 10) Mazungumzo.

Matendo ya jeuri yanaongezeka ulimwenguni kote. Yehova anajua kwamba jeuri tunayoona na kukabili inaweza kutusababishia mahangaiko mengi. Pia anatambua tunahitaji ulinzi. Njia moja ambayo anatulinda ni kupitia Neno lake, Biblia.—Zb 12:​5-7.

Biblia ina hekima ambayo “ni bora kuliko silaha za vita.” (Mhu 9:18) Fikiria jinsi kanuni za Biblia zifuatazo zinavyoweza kutulinda tusiwe waathiriwa wa jeuri.

  • Mhu 4:​9, 10—Epuka kuwa peke yako katika maeneo na hali ambazo si salama

  • Met 22:3—Unapokuwa katika maeneo ya umma uwe macho kuhusu mambo yanayoendelea kukuzunguka

  • Met 26:17—Usijihusishe katika ubishi usiokuhusu

  • Met 17:14—Ondoka katika eneo ikiwa inaonekana kwamba jeuri itaanza. Epuka umati unaojikusanya ili kufanya maandamano

  • Lu 12:15—Usihatarishe kamwe uhai ili kulinda mali zako

Onyesha VIDEO Waige Waaminifu, Si Wasio Waaminifu —Enoko, Si Lameki. Kisha uwaulize wasikilizaji:

Mfano wa Enoko uliathirije maamuzi na mwenendo wa baba huyo kulipokuwa na jeuri?—Ebr 11:5

Katika hali fulani, huenda Mkristo akahisi kuna uhitaji wa kuchukua hatua za kujilinda au kulinda mali yake. Ikiwa ndivyo, atafanya yote anayoweza ili kuepuka kuua na kuwa na hatia ya damu.—Zb 51:14; ona “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” katika gazeti Mnara wa Mlinzi la Julai 2017.

9. Kampeni ya Ukumbusho Itaanza Jumamosi, Machi 2

(Dak. 5) Hotuba itolewe na mzee. Eleza mipango ya kutaniko lenu ya kampeni, hotuba ya pekee, na Ukumbusho. Wakumbushe wahubiri wanaotaka kufanya upainia msaidizi mwezi wa Machi na Aprili kwamba wanaweza kuchagua kutimiza takwa la saa 15.

10. Funzo la Biblia la Kutaniko

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 40 na Sala