Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Februari 3-9

ZABURI 144-146

Februari 3-9

Wimbo 145 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. “Wenye Furaha Ni Watu Ambao Mungu Wao Ni Yehova!”

(Dak. 10)

Yehova huwabariki wale wanaomtegemea (Zb 144:​11-15; w18.04 32 ¶3-4)

Tunashangilia katika tumaini letu (Zb 146:5; w22.10 28 ¶16-17)

Wale ambao Mungu wao ni Yehova watakuwa na furaha milele (Zb 146:10; w18.01 26 ¶19-20)

Tunapomtumikia Yehova kwa uaminifu, tunaweza kuwa na furaha licha ya kuwa na matatizo

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 145:​15, 16—Mistari hii inapaswa kuongozaje jinsi tunavyowatendea wanyama? (it-1 111 ¶9)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Mtu huyo anakuambia kwamba yeye ni mwanafunzi wa chuo kikuu. (lmd somo la 1 jambo kuu la 5)

5. Kufuatia Upendezi

(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Tumia video kutoka kwenye Sanduku la Vifaa vya Kufundishia. (lmd somo la 7 jambo kuu la 4)

6. Hotuba

(Dak. 4) lmd nyongeza A jambo kuu la 7—Kichwa: Mke Anapaswa Kumheshimu Sana Mume Wake. (th somo la 1)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 59

7. Yehova Anataka Uwe na Furaha

(Dak. 10) Mazungumzo.

Yehova ndiye Mungu mwenye furaha. (1Ti 1:11) Ametupatia zawadi nyingi za pekee zinazotuonyesha kwamba anatupenda sana naye anataka tuwe na furaha. (Mhu 3:​12, 13) Fikiria zawadi mbili kati ya hizo—chakula na sauti.

Onyesha VIDEO Uumbaji Unathibitisha Kwamba Yehova Anataka Tuwe na Furaha—Chakula Kitamu na Sauti Zenye Kupendeza. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Zawadi za chakula na sauti zinakusadikishaje kwamba Yehova anataka tuwe na furaha?

Soma Zaburi 32:8. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Kujua kwamba Yehova anataka uwe na furaha kunakuchocheaje kusikiliza mwongozo anaotoa kupitia Biblia na tengenezo lake?

8. Mahitaji ya Kutaniko

(Dak. 5)

9. Funzo la Biblia la Kutaniko

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 85 na Sala