Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Januari 6-12

ZABURI 127-134

Januari 6-12

Wimbo 134 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Wazazi—Endeleeni Kuutunza Urithi Wenu Wenye Thamani

(Dak. 10)

Wazazi wanaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atawasaidia kupata mahitaji ya familia zao (Zb 127:​1, 2)

Watoto ni zawadi yenye thamani kutoka kwa Yehova (Zb 127:3; w21.08 5 ¶9)

Mzoeze kila mtoto kulingana na mahitaji yake (Zb 127:4; w19.12 27 ¶20)

Yehova anafurahi sana wazazi wanapomtegemea na kufanya yote wanayoweza kuwatunza watoto wao

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 128:3—Kwa nini mtunga-zaburi analinganisha wana na machipukizi, au miche, ya mzeituni? (w00 5/15 27 ¶3-5)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) MAHUBIRI YASIYO RASMI. (lmd somo la 1 jambo kuu la 3)

5. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Mtu huyo anataja jambo lisilopatana na fundisho fulani la Biblia. (lmd somo la 5 jambo kuu la 4)

6. Kufanya Wanafunzi

(Dak. 5) lff somo la 16 jambo kuu la 4-5. Zungumza na mwanafunzi wako kuhusu mipango uliyofanya ili aendelee na funzo wakati ambapo hutakuwepo. (lmd somo la 10 jambo kuu la 4)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 13

7. Wazazi—Je, Mnatumia kwa Ufanisi Kifaa Hiki Kilicho na Nguvu Sana?

(Dak. 15) Mazungumzo.

Tengenezo la Yehova limetokeza machapisho na vifaa vingine vingi vya kuwasaidia wazazi kuwafundisha watoto wao kumhusu Yehova. Hata hivyo, kifaa kilicho na nguvu zaidi ambacho wazazi wanaweza kutumia ni mfano wao mzuri.—Kum 6:​5-9.

Yesu alitumia kifaa hicho muhimu kuwafundisha wanafunzi wake.

Soma Yohana 13:​13-15. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Kwa nini unafikiri njia ya Yesu ya kufundisha kupitia mfano wake ilikuwa na matokeo mazuri?

Ukiwa mzazi, matendo yako yanaweza kukazia umuhimu wa mambo unayomfundisha. Pia, mfano wako mzuri utamfanya aheshimu mambo unayofundisha na kumchochea mtoto wako kusikiliza.

Onyesha VIDEO Kuwafundisha Watoto Kupitia Mfano Wetu. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Ndugu na Dada Garcia waliwafundisha binti zao masomo gani muhimu?

  • Video hii inakuchocheaje kuendelea kuwawekea watoto wako mfano mzuri?

8. Funzo la Biblia la Kutaniko

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 73 na Sala