Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Kampeni ya Pekee ya Kutangaza Ufalme wa Mungu Mwezi wa Septemba!

Kampeni ya Pekee ya Kutangaza Ufalme wa Mungu Mwezi wa Septemba!

Mwezi wa Septemba, tutafanya jitihada ya pekee ya kuwaonyesha watu kwamba Ufalme wa Mungu ndio suluhisho pekee la matatizo ya wanadamu. (Mt 24:14) Unaweza kufanya nini ili kushiriki? Katika mwezi huo wasomee watu wengi kadiri iwezekanavyo andiko kuhusu Ufalme wa Mungu. Mtu akipendezwa, mpe nakala ya toleo la watu wote la Mnara wa Mlinzi Na. 2 2020. Kisha fuatia upendezi haraka iwezekanavyo, na ujaribu kuanzisha funzo la Biblia ukitumia broshua Furahia Maisha Milele! Wote wanaotumikia wakiwa mapainia wasaidizi katika mwezi wa Septemba wanaweza kuchagua kutimiza takwa la saa 15 au 30.

Hivi karibuni Ufalme wa Mungu utapondaponda serikali nyingine zote zinazoupinga. (Da 2:44; 1Ko 15:24, 25) Sote na tutumie vizuri fursa hii ya kuonyesha ushikamanifu wetu kwa Yehova na Ufalme wake!