Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Wanafanya Kazi kwa Bidii Ili Kutuhudumia

Wanafanya Kazi kwa Bidii Ili Kutuhudumia

Waangalizi wa mzunguko na wake zao wanajidhabihu kwa upendo ili kutuhudumia. Kama sisi, wao pia wana mahitaji ya kibinafsi na nyakati nyingine wanachoka, wanavunjika moyo, na wanakuwa na mahangaiko. (Yak 5:17) Hata hivyo, kila juma wanakazia fikira kuwatia moyo ndugu na dada katika kutaniko ambalo wanatembelea. Kwa kweli waangalizi wa mzunguko “wanastahili heshima mara mbili.”​—1Ti 5:17.

Mtume Paulo alipopanga kutembelea kutaniko la Roma ili kuwapa “zawadi ya kiroho,” alitazamia kwa hamu nafasi ya kuwa na “ubadilishanaji wa kitia moyo.” (Ro 1:11, 12, maelezo ya chini.) Je, umewahi kufikiria jinsi ya kumtia moyo mwangalizi wenu wa mzunguko na mke wake, ikiwa ameoa?

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA MAISHA YA MWANGALIZI WA MZUNGUKO VIJIJINI, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Waangalizi wa mzunguko na wake zao wanaonyeshaje upendo wa kujidhabihu kwa ajili ya makutaniko?

  • Wewe binafsi umenufaikaje kutokana na jitihada zao?

  • Tunaweza kufanya nini ili kuwatia moyo?