Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kokkinakis v. Greece: Droit réservé

Kuanzia juu kushoto kwenda kulia: West Virginia State Board of Education v. Barnette; Kokkinakis v. Greece; Taganrog LRO and Others v. Russia; Cha and Others v. South Korea

MAISHA YA MKRISTO

“Kuitetea na Kuithibitisha Kisheria Habari Njema”

“Kuitetea na Kuithibitisha Kisheria Habari Njema”

Wapinzani walipojaribu kuwazuia Waisraeli wasijenge upya hekalu, wajenzi hao walifanya yote waliyoweza kuthibitisha haki yao ya kisheria ya kuendelea na kazi hiyo. (Ezr 5:11-16) Vivyo hivyo, Wakristo hufanya yote wawezayo kutetea na kuthibitisha kisheria habari njema. (Flp 1:7) Ili kutimiza hilo, katika mwaka wa 1936 Idara ya Sheria ilianzishwa katika makao makuu ya ulimwenguni pote. Leo, Idara ya Sheria ya Makao Makuu inasimamia kazi ya kutetea masilahi ya Ufalme ulimwenguni pote. Idara hiyo imesaidiaje kazi ya Ufalme na kuwanufaisha watu wa Mungu?

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA KUTEMBELEA IDARA YA SHERIA YA MAKAO MAKUU, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Mashahidi wa Yehova wamekabili changamoto zipi?

  • Tumepata ushindi gani wa kisheria? Toa mfano

  • Kila mmoja wetu anaweza kufanya nini ili “kuitetea na kuithibitisha kisheria habari njema”?

  • Katika tovuti yetu, tunaweza kupata wapi habari za kisheria kuwahusu watu wa Mungu na orodha ya Mashahidi wa Yehova ambao wamefungwa kwa sababu ya imani yao?