Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Yehova Angesemaje?

Yehova Angesemaje?

Kabla ya kufanya maamuzi makubwa au madogo, je, sisi hujiuliza, ‘Yehova angesemaje?’ Ingawa hatutaweza kujua kila kitu kuhusu akili ya Yehova, amefunua mambo mengi katika Neno lake ili kutuwezesha kuwa na vifaa kamili kwa ajili ya “kila kazi njema.” (2Ti 3:16, 17; Ro 11:33, 34) Yesu alifahamu vizuri mapenzi ya Yehova na aliyatanguliza katika maisha yake. (Yoh 4:34) Kwa kumwiga Yesu, na tujitahidi kadiri tuwezavyo kufanya maamuzi ambayo yanampendeza Yehova.—Yoh 8:28, 29; Efe 5:15-17.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA ENDELEA KUFAHAMU MAPENZI YA YEHOVA (LAW 19:18), KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Kwa nini tunapaswa kutumia kanuni za Biblia maishani mwetu?

  • Ni kanuni gani za Biblia tunazoweza kutumia tunapochagua muziki?

  • Ni kanuni gani za Biblia tunazopaswa kutumia tunapochagua mavazi na mapambo?

  • Ni katika sehemu gani nyingine za maisha tunazopaswa kutumia kanuni za Biblia?

  • Tunaweza kuboreshaje uwezo wetu wa kufahamu mapenzi ya Yehova?

Maamuzi yangu yanafunua nini kuhusu uhusiano wangu na Yehova?