Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | WAGALATIA 4-6

“Tukio la Mfano” Linalotuelimisha

“Tukio la Mfano” Linalotuelimisha

4:24-31

Mtume Paulo alitumia ‘tukio hili la mfano’ kuonyesha ubora wa agano jipya kwa kulinganishwa na Agano la Sheria. Chini ya uangalizi wa Kristo na warithi wenzake, wanadamu wote wana taraja la kuwekwa huru kutokana na dhambi, kutokamilika, huzuni, na kifo.—Isa 25:8, 9.

 

HAGARI​—YULE KIJAKAZI

Taifa halisi la Israeli chini ya agano la Sheria, Yerusalemu lilikuwa mji mkuu

SARA​—YULE MWANAMKE HURU

Yerusalemu la juu, sehemu ya kimbingu ya tengenezo la Mungu

“WATOTO” WA HAGARI

Wayahudi (wakiwa wameunganishwa na Yehova kupitia agano la Sheria) walimnyanyasa na kumkataa Yesu

“WATOTO” WA SARA

Kristo na wale Wakristo 144,000 waliotiwa mafuta kwa roho takatifu

WATUMWA WA AGANO LA SHERIA

Sheria iliwakumbusha Waisraeli kwamba walikuwa watumwa wa dhambi

AGANO JIPYA LINAANDAA UHURU

Imani katika thamani ya dhabihu ya Kristo ilifanya wapate uhuru kutoka kwa hukumu ya Sheria