Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | AYUBU 11-15

Ayubu Alikuwa na Uhakika Kwamba Kungekuwa na Ufufuo

Ayubu Alikuwa na Uhakika Kwamba Kungekuwa na Ufufuo

Ayubu alionyesha imani kuwa Mungu ana uwezo wa kumfufua

14:7-9, 13-15

  • Ayubu alitumia mfano wa mti, labda ule wa mzeituni, ili kuonyesha uwezo wa Mungu wa kumfufua

  • Mizizi ya mzeituni inaenea sana hivi kwamba inaweza kuusadia mti huo kukua tena hata kama shina la mti huo limekatwa. Ikiwa mizizi hiyo iko hai, basi mti huo utachipuka tena

  • Mvua inaponyesha baada ya kipindi kirefu cha ukame, kisiki cha mzeituni kinaweza kuchipua mmea kutoka kwenye mizizi, na kutokeza “matawi kama mmea mpya”