Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Karibisha Wageni

Karibisha Wageni

Tarehe 23 mwezi Machi, wageni milioni 12 au zaidi wanatarajiwa kuhudhuria Ukumbusho. Watakaohudhuria watafurahia kujifunza mambo mengi sana msemaji atakapozungumzia kuhusu fidia ambayo ni zawadi kutoka kwa Yehova na baadhi ya baraka tutakazopata wakati ujao! (Isa 11:6-9; 35:5, 6; 65:21-23; Yoh 3:16) Hata hivyo, katika tukio hilo la pekee wahudhuriaji watanufaika na mambo mengine zaidi. Sisi sote tunaweza kufanya sehemu yetu kwa kuwakaribisha wageni kwa shauku. (Ro 15:7) Tunaweza kutumia mapendekezo yafuatayo.

  • Badala ya kwenda kuketi moja kwa moja na kusubiri mkutano uanze, wakaribishe wageni na wale wasiotenda kwa kutabasamu na kuwasalimu kwa shauku

  • Unapofurahia ushirika pamoja na wageni unaowafahamu ambao umewaalika, uwe makini kuwakaribisha wengine ambao huenda walialikwa wakati wa kampeni. Waalike wageni waketi karibu nawe na usome Biblia na kuimba nao

  • Baada ya hotuba, uwe tayari kujibu maswali yoyote watakayouliza. Ikiwa mtalazimika kuondoka haraka kwa sababu kutaniko lingine litafanya Ukumbusho mara tu baada ya kutaniko lenu kumaliza, fanya mipango ya kumtembelea aliyependezwa bila kukawia. Ikiwa huna namba zake za simu au anwani yake, unaweza kumwambia: “Ningependa kujua maoni yako kuhusu mkutano huu. Kuna njia yoyote ninayoweza kuwasiliana nawe?”