Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi

Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi

MNARA WA MLINZI

Swali: Kwa maoni yako, ni zawadi gani kubwa zaidi ambayo Mungu amewahi kutupatia?

Andiko: Yoh 3:16

Pendekezo: Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linaonyesha kwa nini Mungu alimtuma Yesu duniani afe kwa ajili yetu na jinsi tunavyoweza kuonyesha tunaithamini zawadi hiyo.

UFALME WA MUNGU NI NINI?

Swali: [Onyesha ukurasa wa kwanza wa trakti hiyo.] Ungejibuje swali hili? Unafikiri Ufalme wa Mungu ni kitu kilicho moyoni? kitu kisicho halisi au mfano? au ni serikali iliyo mbinguni?

Andiko: Da 2:44; Isa 9:6

Pendekezo: Trakti hii inaonyesha mambo yatakayotimizwa na Ufalme wa Mungu.

MWALIKO WA UKUMBUSHO

Pendekezo: Tunawakaribisha watu kwenye tukio muhimu sana. [Mpe mwaliko.] Aprili 11, mamilioni ya watu ulimwenguni pote watakutana pamoja kukumbuka kifo cha Yesu na kusikiliza hotuba ya Biblia bila malipo itakayotuonyesha jinsi kifo cha Yesu kinavyoweza kutunufaisha. Mwaliko huu unaonyesha wakati na mahali ambapo ukumbusho huo utafanywa katika eneo letu. Tunatumaini utahudhuria.

ANDIKA UTANGULIZI WAKO

Ukitumia mpangilio ulioonyeshwa katika mifano iliyotangulia tayarisha utangulizi wako kwa ajili ya utumishi.