Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Jinsi ya Kutumia Broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?

Jinsi ya Kutumia Broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?

Broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo? ilitayarishwa ili kujifunza na wanafunzi wa Biblia mwanzoni au mwishoni mwa kila kipindi cha funzo la Biblia. * Somo la 1 hadi la 4 linawasaidia wanafunzi kuelewa sisi ni watu wa aina gani, somo la 5 hadi la 14 linawasaidia kujifunza kuhusu utendaji wetu, na somo la 15 hadi la 28 linawaonyesha jinsi tengenezo letu linavyofanya kazi. Ni vizuri kuzungumzia masomo hayo kama yanavyofuatana, lakini ikiwa somo fulani linahusiana na mahitaji ya mwanafunzi ya wakati huo mnaweza kulizungumzia kwanza. Kila somo lina urefu wa ukurasa mmoja tu na linaweza kuzungumziwa kwa dakika tano hadi kumi.

  • Anza kwa kukazia swali lililo kwenye kichwa cha somo

  • Someni somo lote pamoja. Mnaweza kusoma mafungu yote kwanza, au msome sehemu moja na kuizungumzia kabla ya kusoma sehemu inayofuata

  • Zungumzieni sehemu mliyosoma. Tumia maswali yanayopatikana katika sehemu ya chini ya ukurasa na picha. Someni na mzungumzie maandiko yaliyotajwa kulingana na uhitaji. Kazia kwamba vichwa vidogo vya habari vilivyoandikwa kwa herufi nzito vinajibu swali kwenye kichwa cha somo hilo

  • Ikiwa somo lina sanduku lenye kichwa “Pata Kujua Mengi Zaidi” soma na mwanafunzi na umtie moyo afuate mapendekezo yaliyotolewa

^ fu. 3 Toleo la mtandaoni ndilo toleo la karibuni zaidi la broshua hiyo.