Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Jinsi ya Kutumia Broshua Msikilize Mungu

Jinsi ya Kutumia Broshua Msikilize Mungu

Broshua Msikilize Mungu imekusudiwa kwa ajili ya watu walio na matatizo ya kusoma, ili kuwafundisha kuhusu kweli za msingi za Biblia kwa kutumia picha. Kila somo lina kurasa mbili ambazo zina picha zilizotayarishwa kwa makini na vishale vya kuelekeza kutoka picha moja hadi nyingine.

Broshua Msikilize Mungu Uishi Milele ina picha sawa na zile zilizo katika broshua Msikilize Mungu, lakini broshua Msikilize Mungu Uishi Milele ina maandishi mengi zaidi na inaweza kutumiwa na wanafunzi ambao wana uwezo fulani wa kusoma. Wahubiri hupendelea kuitumia kama nakala ya mwalimu, wanafunzi wao wanapotumia broshua Msikilize Mungu. Kurasa nyingi zina sanduku lililo na habari ya ziada ambayo inaweza kuzungumziwa ikitegemea uwezo wa mwanafunzi.

Unaweza kutoa broshua hizo wakati wowote, hata ikiwa si toleo la mwezi. Unapoongoza funzo la Biblia, tumia picha kueleza masimulizi ya Biblia. Uliza maswali ili umhusishe mwanafunzi katika mazungumzo na ili uhakikishe anaelewa habari hiyo. Someni na mzungumzie maandiko yaliyo chini ya kila ukurasa. Baada ya kumaliza broshua hiyo, jifunzeni kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? au Biblia Inatufundisha Nini? ili umsaidie mwanafunzi wako afanye maendeleo na kubatizwa.