Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Isaidie Familia Yako Kumkumbuka Yehova

Isaidie Familia Yako Kumkumbuka Yehova

Yeremia aliagizwa awaonye Wayahudi kuhusu uharibifu uliokuwa ukija kwa sababu walikuwa wamemsahau Mungu wao, Yehova. (Yer 13:25) Taifa hilo lilifikiaje hali hiyo yenye kusikitisha kiroho? Hali ya kiroho ya familia za Israeli ilikuwa imeharibika. Ni wazi kwamba vichwa vya familia hawakuwa wakifuata mwongozo wa Yehova ulio kwenye Kumbukumbu la Torati 6:5-7.

Leo, familia imara kiroho husaidia sana kuimarisha makutaniko yetu. Vichwa vya familia wanaweza kusaidia familia zao kumkumbuka Yehova kwa kuwa na programu ya Ibada ya Familia ya kila juma na iliyojaa maana. (Zb 22:27) Baada ya kutazama video yenye kichwa Maneno Haya . . . Lazima Yawe Moyoni Mwako”—Mahojiano ya Familia, jibu maswali haya:

  • Baadhi ya familia zimefauluje kukabiliana na changamoto zinazoathiri ibada ya familia?

  • Ni thawabu gani zinazopatikana kwa kuwa na Ibada ya Familia ya kila juma na iliyojaa maana?

  • Mimi ninakabili changamoto zipi kuhusiana na ibada ya familia, na nimepanga kuzishughulikiaje?