DAFTARI LA MKUTANO WA HUDUMA NA MAISHA Machi 2018
Mapendekezo ya Kuanzisha Mazungumzo
Mazungumzo yanayotegemea kampeni ya kuwaalika watu kwenye ukumbusho na maswali yafuatayo: Kwa nini Yesu alikufa? Fidia inatimiza nini?
HAZINA ZA NENO LA MUNGU
“Yeyote Anayetaka Kuwa Mkubwa Kati Yenu Lazima Awe Mhudumu Wenu”
Je, katika ibada yetu tunajihusisha tu na mambo ambayo yatatufanya tutambuliwe na kusifiwa na wengine? Mara nyingi mhudumu mnyenyekevu hufanya kazi zinazotambuliwa tu na Yehova Mungu.
HAZINA ZA NENO LA MUNGU
Tii Zile Amri Mbili Kuu Zaidi
Yesu alisema nini kuhusu zile amri kuu mbili zinazopatikana katika Biblia? Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunatii amri hizo?
MAISHA YA MKRISTO
Jinsi ya Kusitawisha Upendo kwa Mungu na Jirani
Tunapaswa kumpenda Mungu na jirani. Njia moja muhimu ya kusitawisha upendo huo ni kupitia kusoma Biblia kila siku.
HAZINA ZA NENO LA MUNGU
Endelea Kuwa Macho Kiroho Katika Siku za Mwisho
Watu wengi leo wameruhusu shughuli za kawaida za maisha ziwazuie kufanya mambo ya kiroho. Wakristo walio macho kiroho wanatofautianaje na watu hao?
MAISHA YA MKRISTO
Tuko Karibu Sana na Mwisho wa Mfumo Huu wa Mambo
Maneno ya Yesu yanaonyeshaje kwamba tunaishi karibu sana na mwisho wa mfumo huu wa mambo? Swali hilo na mengine mengi yanajibiwa katika video yenye kichwa Tuko Karibu Sana na Mwisho wa Mfumo Huu wa Mambo.
HAZINA ZA NENO LA MUNGU
“Endeleeni Kukesha”
Katika mfano wa Yesu wa mabikira kumi, ni nani anayewakilisha bwana harusi, mabikira wenye busara, na mabikira wapumbavu? Na mfano huo unakuhusuje?
MAISHA YA MKRISTO
Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kuwafundisha Wanafunzi Wetu Kujitayarisha
Mapema sana, tunapaswa kumsaidia mwanafunzi wetu asitawishe mazoea ya kujitayarisha kwa ajili ya funzo. Tunaweza kumsaidiaje?