Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma​—Kuwafundisha Wanafunzi Wetu Kujitayarisha

Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma​—Kuwafundisha Wanafunzi Wetu Kujitayarisha

KWA NINI NI MUHIMU: Wanafunzi wa Biblia wanapojitayarisha, wanaweza kuelewa na kukumbuka upesi zaidi mambo tunayowafundisha. Kadiri wanavyoelewa na kukumbuka, ndivyo watakavyofanya maendeleo haraka zaidi. Hata baada ya kubatizwa, watahitaji kujitayarisha kwa ajili ya mikutano na huduma ili ‘waendelee kukesha.’ (Mt 25:13) Hivyo, kujua jinsi ya kujifunza na kuwa na ratiba nzuri ya kujifunza kutawanufaisha katika maisha yao yote. Tangu mwanzo, tunapaswa kuwasaidia wanafunzi wetu kusitawisha zoea la kujitayarisha kwa ajili ya funzo la Biblia.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Weka mfano mzuri. (Ro 2:21) Jitayarishe kwa ajili ya kila funzo ukimfikiria mwanafunzi wako. (km 11/15 3) Mruhusu aone chapisho lako ambalo umetayarisha.

  • Mtie moyo atayarishe. Mara tu funzo linapokuwa la kawaida, mjulishe kwamba matayarisho ni sehemu ya mpango wa funzo la Biblia, na ueleze manufaa. Toa mapendekezo yanayofaa ya jinsi anavyoweza kutenga wakati ili kujitayarisha. Wakati wa funzo walimu fulani humruhusu mwanafunzi atumie chapisho la mwalimu ambalo limepigwa mistari ili kumsaidia aone faida za kufanya hivyo. Mpongeze anapojitayarisha

  • Mwonyeshe jinsi ya kujitayarisha. Mapema sana, walimu fulani hutumia kipindi kizima cha funzo ili kumwonyesha mwanafunzi jinsi ya kujitayarisha