Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | WAROMA 12-14

Kuonyesha Upendo wa Kikristo Kunamaanisha Nini?

Kuonyesha Upendo wa Kikristo Kunamaanisha Nini?

12:10, 17-21

Mtu anapotukosea, mbali tu na kutolipiza kisasi, upendo wa Kikristo utatuchochea kufanya mengi zaidi. “Ikiwa adui yako ana njaa, mlishe; ikiwa ana kiu, mpe kitu anywe; kwa maana kwa kufanya hivyo utakusanya makaa ya mawe yanayowaka juu ya kichwa chake.” (Ro 12:20) Fadhili tunazomwonyesha mtu anayetutendea kwa njia isiyofaa zinaweza kumfanya mtu huyo ajutie matendo yake.

Ulihisije ulipotendewa kwa fadhili na mtu fulani uliyemuumiza bila kukusudia?