Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Nitamkaribisha Nani?

Nitamkaribisha Nani?

Kila mwaka tunafanya jitihada za pekee kuwaalika watu katika eneo letu kuhudhuria Ukumbusho. Wengi wao ni watu tusiowafahamu. Tunapaswa pia kualika watu tunaowafahamu. Kuna uwezekano mkubwa wa mtu kuhudhuria Ukumbusho anapopokea mwaliko kutoka kwa mtu anayemfahamu. (yb08 11 ¶3; 14 ¶1) Wewe unaweza kumwalika nani?

  • Watu wa ukoo

  • Wafanyakazi wenzako au wanafunzi wenzako

  • Majirani

  • Ziara za kurudia na watu uliojifunza nao zamani au unaojifunza nao sasa

Pia, wazee watawakaribisha wasiotenda. Vipi ikiwa mtu unayetaka kumwalika haishi katika eneo lenu? Ili ujue muda na mahali Ukumbusho utakapofanyika karibu na mahali anapoishi, bofya kitufe cha KUTUHUSU katika ukurasa wa mwanzo wa tovuti ya jw.org, kisha bofya “Ukumbusho.” Unapojiandaa kwa ajili ya Ukumbusho wa mwaka huu, wafikirie wale unaoweza kuwaalika, kisha uwaalike wewe binafsi.