Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Chagua Marafiki Wako kwa Hekima

Chagua Marafiki Wako kwa Hekima

Kilichowapata Waisraeli kwenye nyanda za Moabu ni kielelezo cha kuonya kwa Wakristo. (1Ko 10:6, 8, 11) Baadhi ya Waisraeli walishawishiwa kutenda dhambi nzito kwa sababu walianza kushirikiana na wanawake Wamoabu waliokuwa na maadili mapotovu na walioabudu sanamu. Hilo lilisababisha madhara makubwa. (Hes 25:9) Tumezungukwa na wafanyakazi, wanafunzi, majirani, watu wa ukoo, na marafiki ambao hawamwabudu Yehova. Tunaweza kujifunza nini kutokana na simulizi hili la Biblia kuhusu hatari za kushirikiana kwa ukaribu na watu kama hao?

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA VIELELEZO VYA KUONYA LEO—KISEHEMU, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Zimri na wengine walimwonyesha Yamini mtazamo gani mbaya?

  • Finehasi alimsaidiaje Yamini kuwa na mtazamo unaofaa?

  • Kuna tofauti gani kati ya kumwonyesha mtu ambaye si mwamini urafiki na kuwa rafiki yake?

  • Kwa nini tunapaswa kuwa waangalifu tunapochagua marafiki hata kutanikoni?

  • Kwa nini tunapaswa kuepuka vikundi vya mazungumzo kwenye mitandao ya kijamii na watu tusiowafahamu?