Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Fanya Maamuzi Yenye Hekima Kuhusu Kileo

Fanya Maamuzi Yenye Hekima Kuhusu Kileo

Wakristo wote wanapaswa kuwa na sifa ya kujizuia inapohusu kileo. (Met 23:20, 29-35; 1Ko 6:9, 10) Ikiwa Mkristo ataamua kunywa, anapaswa kufanya hivyo kwa kiasi. Anapaswa kuepuka kutegemea kileo na kuwakwaza wengine. (1Ko 10:23, 24; 1Ti 5:23) Kwa kweli, hakuna mtu anayepaswa kushinikizwa kutumia kileo, hasa vijana.

TAZAMENI VIDEO YA VIBONZO KWENYE UBAO FIKIRIA MADHARA KABLA YA KUNYWA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Kwa nini Wakristo wote wanapaswa kutii sheria zinazohusu kunywa kileo?—Ro 13:1-4

  • Kwa nini hatupaswi kuwaruhusu wengine watushinikize kunywa kileo?—Ro 6:16

  • Tunaweza kuepukaje mitego inayohusu kileo?