Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Endelea Kuwa Tayari Katika Sehemu ya Mwisho ya “Siku za Mwisho”

Endelea Kuwa Tayari Katika Sehemu ya Mwisho ya “Siku za Mwisho”

Kadiri tunavyovumilia hali ngumu katika sehemu ya mwisho ya “siku za mwisho,” tunatarajia kwamba matatizo yatazidi kuongezeka. (2Ti 3:1; nwtsty habari za utafiti Mt 24:8) Janga la asili linapotokea, mara nyingi watu wa Yehova hupokea mwongozo kwa wakati na unaookoa uhai. Hivyo, tunahitaji kutii na kujitayarisha sasa kiroho na kimwili ili tuokoke wakati huo.Lu 16:10.

  • Jitayarishe kiroho: Dumisha ratiba nzuri. Jifunze njia mbalimbali za kushiriki katika huduma. Usiwe na hofu hata ikiwa utatenganishwa kwa muda mfupi na wengine kutanikoni. (Isa 30:15) Hujatenganishwa na Yehova na Yesu.—od 176 ¶15-17

  • Jitayarishe kimwili: Mbali na mikoba ya dharura, kila familia inapaswa kuwa na chakula cha ziada, maji, dawa, na mahitaji mengine ikiwa itakuwa lazima kukaa ndani kwa muda mrefu.—Met 22:3; g17.5 4, 6

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA JE, UMEJITAYARISHA KUKABILIANA NA MAJANGA YA ASILI? KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Tunaweza kujitayarishaje kiroho kwa ajili ya msiba?

  • Kwa nini tunapaswa . . .

    • kudumisha mawasiliano mazuri na wazee?

    • kutayarisha begi la (mkoba wa) dharura?

    • kuzungumzia aina ya misiba inayoweza kutokea na hatua mnayopaswa kuchukua katika kila hali?

  • Ni njia gani tatu tunazoweza kuwasaidia wengine wanapopatwa na msiba?

JIULIZE, ‘Ugonjwa wa virusi vya corona (COVID-19) umenifundisha masomo gani kuhusu kuwa tayari kwa ajili ya hali ya dharura?’