Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Tumia Furahia Maisha Milele! Kujenga Imani Katika Yehova na Yesu

Tumia Furahia Maisha Milele! Kujenga Imani Katika Yehova na Yesu

Ili kumpendeza Mungu, wanafunzi wa Biblia wanapaswa kusitawisha imani yenye nguvu. (Ebr 11:6) Tunaweza kuwasaidia kufanya hivyo kwa kutumia kitabu Furahia Maisha Milele! Kitabu hicho cha kujifunzia kina maandiko muhimu, kinatoa sababu za wazi, maswali yanayofaa, video zenye kuchochea, na picha maridadi. Tunapowasaidia wanafunzi kusitawisha sifa za Kikristo na uhusiano pamoja na Mungu, tunajenga kwa vifaa visivyoshika moto.​—1Ko 3:12-15.

Ni vigumu kwa watu fulani kufikiria kuwa rafiki ya Mungu, kwa kuwa hawawezi kumwona. Kwa hiyo, tunahitaji kuwasaidia wamjue Mungu na kumtumaini.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA JENGA IMANI KATIKA YEHOVA KWA KUTUMIA CHAPISHO “FURAHIA MAISHA MILELE!” KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Ni nini kinachoonyesha kwamba dada huyo alikuwa amejitayarisha vizuri kwa ajili ya funzo?

  • Alitumiaje maswali machache ya ziada yaliyochaguliwa vizuri ili kumfanya mwanafunzi aeleze mawazo yake kuhusu Isaya 41:10, 13?

  • Mwanafunzi aliathiriwaje na video na mistari hiyo ya Biblia?

Watu wengi hawaelewi maana ya fidia, au hawaioni kuwa zawadi ya kibinafsi kutoka kwa Mungu. (Ga 2:20) Hivyo, lazima tuwasaidie kujenga imani katika dhabihu ya fidia ya Yesu.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA JENGA IMANI KATIKA YESU KWA KUTUMIA CHAPISHO “FURAHIA MAISHA MILELE!” KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Ni nini kinachoonyesha kwamba ndugu huyo alikuwa amejitayarisha vizuri kwa ajili ya funzo?

  • Alifanyaje habari iliyo kwenye sehemu ya “Chunguza Zaidi” imfae mwanafunzi?

  • Kwa nini ni muhimu kusali kwa ajili ya mwanafunzi?