Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

“Upendo . . . Haushangilii Ukosefu wa Uadilifu”

“Upendo . . . Haushangilii Ukosefu wa Uadilifu”

Katika utendaji wao wote, Wakristo wa kweli hujitahidi kuongozwa na upendo. Upendo “haushangilii ukosefu wa uadilifu.” (1Ko 13:4, 6) Hivyo, tunaepuka burudani inayotukuza mambo kama vile ukosefu wa maadili na jeuri. Pia, hatushangilii mambo mabaya yanapowapata watu wengine, hata wale ambao wamewahi kutuumiza.—Met 17:5.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA KUMBUKA JINSI UPENDO ULIVYO​—HAUSHANGILII UKOSEFU WA UADILIFU, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Daudi alitendaje alipogundua kwamba Sauli na Yonathani wamekufa?

  • Daudi alitunga wimbo gani wa maombolezo kwa ajili ya Sauli na Yonathani?

  • Kwa nini Daudi hakushangilia Sauli alipokufa?