MAISHA YA MKRISTO
“Upendo . . . Haushangilii Ukosefu wa Uadilifu”
Katika utendaji wao wote, Wakristo wa kweli hujitahidi kuongozwa na upendo. Upendo “haushangilii ukosefu wa uadilifu.” (1Ko 13:4, 6) Hivyo, tunaepuka burudani inayotukuza mambo kama vile ukosefu wa maadili na jeuri. Pia, hatushangilii mambo mabaya yanapowapata watu wengine, hata wale ambao wamewahi kutuumiza.—Met 17:5.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA KUMBUKA JINSI UPENDO ULIVYO—HAUSHANGILII UKOSEFU WA UADILIFU, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
-
Daudi alitendaje alipogundua kwamba Sauli na Yonathani wamekufa?
-
Daudi alitunga wimbo gani wa maombolezo kwa ajili ya Sauli na Yonathani?
-
Kwa nini Daudi hakushangilia Sauli alipokufa?