Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Je, Uko Tayari Kukabiliana na Misukosuko ya Kijamii?

Je, Uko Tayari Kukabiliana na Misukosuko ya Kijamii?

Kadiri mwisho wa mfumo huu unavyokaribia, tunatarajia kwamba misukosuko ya kijamii, ugaidi, na vita vitaongezeka. (Ufu 6:4) Tunaweza kujitayarishaje kwa ajili ya hali ngumu za wakati ujao?

  • Jitayarishe kiroho: Tafuta kanuni na masimulizi ya Biblia ambayo yataimarisha tumaini lako katika Yehova na tengenezo lake na ambayo yatakusaidia kudumisha msimamo wa kutounga mkono upande wowote. (Met 12:5; jr 125-126 ¶23-24) Sasa ndio wakati wa kuimarisha urafiki pamoja na wengine ndani ya kutaniko.​—1Pe 4:7, 8

  • Jitayarishe kimwili: Pangeni jinsi ya kuhakikisha mko salama ikiwa hamwezi kutoka nyumbani na mhifadhi mahitaji muhimu. Pia, pangeni mambo mtakayofanya ikiwa mtalazimika kuondoka nyumbani. Kagueni vitu vilivyo ndani ya mkoba wa dharura, na mtie ndani pesa na vitu vya kujikinga kama vile glavu na barakoa. Fahamu jinsi ya kuwasiliana na wazee, na uwe na uhakika wao wanafahamu jinsi ya kuwasiliana nawe.​—Isa 32:2; g17.5 3-7

Wakati wa msukosuko, dumisha ratiba yako ya kiroho. (Flp 1:10) Epuka kuhamahama isipokuwa iwe lazima. (Mt 10:16) Shiriki na wengine chakula na mahitaji mengine.​—Ro 12:13.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA JE, UMEJITAYARISHA KUKABILIANA NA MAJANGA? KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Yehova anaweza kutusaidiaje wakati wa majanga?

  • Tunaweza kuchukua hatua zipi zinazofaa ili kujitayarisha?

  • Tunaweza kuwasaidiaje wengine ambao wameathiriwa na majanga?