Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Jilinde Dhidi ya Uasi-Imani

Jilinde Dhidi ya Uasi-Imani

Mara nyingi, Shetani na walio chini ya uvutano wake huchanganya mambo ya kweli na ya uwongo wakijaribu kudhoofisha imani yetu. (2Ko 11:3) Kwa mfano, Waashuru walitumia kweli nusunusu na uwongo ili kuwavunja moyo watu wa Yehova. (2Nya 32:10-15) Waasi-imani hutumia mbinu kama hizo leo. Tunapaswa kuwa na maoni gani kuhusu mafundisho ya waasi-imani? Yaone kuwa sumu hatari! Kamwe usiyasome, usijaribu kuyarekebisha, wala kumweleza mtu mwingine. Tambua upesi habari iliyokusudiwa kukufanya uwe na shaka kumhusu Yehova na tengenezo lake—na uikatae kabisa!—Yud 3, 4.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA MFANYE PIGANO KALI KWA AJILI YA IMANI”!—KISEHEMU, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Kwa nini tunahitaji kuwa makini ikiwa tunatumia vituo vya Intaneti vinavyowaruhusu watu kuwa na mazungumzo?

  • Tunaweza kufuataje ushauri wa Waroma 16:17?