Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

“Je, Unatumia Vizuri Biblia Iliyorekodiwa?”

“Je, Unatumia Vizuri Biblia Iliyorekodiwa?”

Biblia iliyorekodiwa ni nini? Biblia iliyorekodiwa ni rekodi ya usomaji wa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya iliyorekebishwa. Inatolewa hatua kwa hatua katika lugha nyingi kadiri iwezekanavyo. Jambo moja la pekee ni kwamba Biblia iliyorekodiwa inatumia sauti tofauti kwa ajili ya kila mhusika wa Biblia. Maneno yamesomwa kwa mkazo na hisia inayofaa ili kuwasilisha ujumbe wa Biblia kwa usahihi.

Baadhi ya watu wamenufaikaje kutokana na Biblia iliyorekodiwa? Wengi wanaosikiliza kwa ukawaida Biblia iliyorekodiwa wanafurahia jinsi inavyofanya Neno la Mungu kuwa halisi. Wanahisi kwamba kwa kumsikia msomaji tofauti wa kila mhusika wa Biblia, wanaweza kuwazia matukio ya Biblia kwa njia nzuri zaidi na kuelewa vizuri zaidi mambo yaliyoandikwa. (Met 4:5) Pia wengi wameona kwamba kusikiliza Biblia iliyorekodiwa kunawatuliza wanapokuwa na mahangaiko.—Zb 94:19.

Kusikiliza Neno la Mungu likisomwa kwa sauti kunaweza kuwa na manufaa makubwa maishani mwetu. (2Nya 34:19-21) Iwapo Biblia iliyorekodiwa inapatikana ikiwa nzima au kwa sehemu katika lugha unayoelewa, je, unaweza kupanga kwamba kuisikiliza kuwe sehemu ya ratiba yako ya kiroho?

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA KUTOKEZWA KWA BIBLIA ILIYOREKODIWA—KISEHEMU, KISHA MJIBU SWALI LIFUATALO:

Ni nini kinachokuvutia kuhusu kutokezwa kwa Biblia iliyorekodiwa?