Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mei 20-26

ZABURI 40-41

Mei 20-26

Wimbo 102 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Manufaa ya Kuwasaidia Wengine

(Dak. 10)

Kuwasaidia wengine kunatuletea furaha (Zb 41:1; w18.08 22 ¶16-18)

Yehova huwasaidia wale wanaowasaidia wengine (Zb 41:​2-4; w15 12/15 24 ¶7)

Tunamletea Yehova sifa tunapowasaidia wengine (Zb 41:13; Met 14:31; w17.09 12 ¶17)

JIULIZE, ‘Je, kuna mtu katika kutaniko langu anayehitaji kusaidiwa kufahamu jinsi ya kutumia JW Library vizuri zaidi?’

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 40:​5-10—Sala ya Daudi inatusaidiaje kutambua cheo cha Yehova akiwa Mwenye Enzi Kuu? (it-2 16)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Anzisha mazungumzo na mtu anayeonekana kuwa mwenye furaha. (lmd somo la 2 jambo kuu la 3)

5. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Anzisha mazungumzo na mtu anayeonekana kuwa mwenye huzuni. (lmd somo la 3 jambo kuu la 5)

6. Kufanya Wanafunzi

(Dak. 5) lff somo la 14 jambo kuu la 6. Zungumzia jambo moja kutoka kwenye makala yenye kichwa “Msifu Yehova Katika Kutaniko” iliyo katika sehemu ya “Chunguza Zaidi” pamoja na mwanafunzi anayesitasita kushiriki katika mikutano. (th somo la 19)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 138

7. Watendee Mema Wenye Umri Mkubwa

(Dak. 15) Mazungumzo.

Yehova anathamini sana kazi ambayo ndugu na dada wenye umri mkubwa wanafanya kutanikoni. Sisi pia tunathamini kazi yao. (Ebr 6:10) Kwa miaka mingi, wamekuwa wakiwafundisha, kuwazoeza, na kuwatia moyo waabudu wenzao. Bila shaka, wewe unakumbuka jinsi walivyokusaidia. Unaweza kuwaonyeshaje kwamba unathamini yote ambayo wamefanya na wanayoendelea kufanya katika kutaniko?

Onyesha VIDEO ‘Tuwatendee Ndugu Zetu Mema.’ Kisha waulize wasikilizaji:

  • Ji-Hoon alijifunza nini kutoka kwa Ndugu Ho-jin Kang?

  • Unathamini jambo gani kuwahusu wenye umri mkubwa katika kutaniko lenu?

  • Tunaweza kujifunza somo gani kutokana na mfano wa Msamaria mwema?

  • Kulikuwa na manufaa gani Ji-Hoon alipowahusisha wengine alipokuwa akimsaidia Ndugu Ho-jin Kang?

Tunapofikiria wenye umri mkubwa katika kutaniko letu wana mahitaji gani, tunaweza kupata njia nyingi za kuwasaidia. Unapoona uhitaji, fikiria unaweza kufanya nini ili kuushughulikia.—Yak 2:​15, 16.

Soma Wagalatia 6:10. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Ni katika njia zipi unaweza ‘kuwatendea mema’ wenye umri mkubwa katika kutaniko lenu?

8. Funzo la Biblia la Kutaniko

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 8 na Sala