Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mei 27–Juni 2

ZABURI 42-44

Mei 27–Juni 2

Wimbo 86 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Nufaika Kikamili Kutokana na Mafundisho ya Yehova

(Dak. 10)

Tumia nafasi zote unazopata za kumwabudu Yehova pamoja na wengine, ikiwezekana fanya hivyo uso kwa uso (Zb 42:​4, 5; w06 6/1 9 ¶4)

Sali kabla ya kujifunza Neno la Mungu (Zb 42:8; w12 1/15 15 ¶2)

Iruhusu Biblia ikuongoze katika kila jambo unalofanya maishani (Zb 43:3)

Mafundisho ya Yehova yanatuimarisha tukabiliane na majaribu na kutuwezesha kuishi kupatana na wakfu wetu.—1Pe 5:10; w16.09 5 ¶11-12.

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 44:19—Huenda maneno “mahali ambapo mbwamwitu wanakaa” yanamaanisha nini? (it-1 1242)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwalike ajifunze Biblia. (lmd somo la 5 jambo kuu la 5)

5. Kufuatia Upendezi

(Dak. 5) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwalike mwenye nyumba asikilize hotuba ya watu wote ifuatayo. Tumia video Ni Nini Hutendeka Katika Jumba la Ufalme? (lmd somo la 7 jambo kuu la 5)

6. Hotuba

(Dak. 3) lmd nyongeza A jambo kuu la 4—Kichwa: Kila Mtu Atakuwa na Afya Kamilifu. (th somo la 2)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 21

7. Fanya Maamuzi Yenye Hekima Kuhusu Kazi na Elimu

(Dak. 15) Mazungumzo.

Vijana, je, mmepanga mtakachofanya baada ya kumaliza shule ya sekondari? Huenda tayari unafikiria kufanya kazi ambayo itakuruhusu kuwa painia. Au huenda ukawa unafikiria kupata mafunzo fulani ambayo yatakusaidia kupata ustadi, leseni, au diploma itakayokuwezesha kupata kazi ya aina hiyo. Bila shaka unasisimka kufikiria kuhusu mambo hayo! Hata hivyo, huenda ukahisi umelemewa kwa sababu ya maamuzi unayopaswa kufanya au ukahisi una mkazo kwa sababu ungependa kufanya uamuzi utakaowafurahisha wengine. Ni nini kinachoweza kukusaidia kufanya maamuzi yenye hekima?

Soma Mathayo 6:​32, 33. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Kwa nini ni muhimu kujiwekea miradi hususa ya kiroho kabla ya kufanya maamuzi muhimu kuhusu kazi na elimu?

  • Wazazi wanaweza kuwasaidiaje watoto wao kutumia ushauri ulio kwenye Mathayo 6:​32, 33?—Zb 78:​4-7

Uwe mwangalifu usiruhusu tamaa ya kuwa na usalama wa kifedha au umashuhuri iathiri maamuzi yako. (1Yo 2:​15, 17) Kumbuka kwamba kuwa na mali nyingi kunaweza kufanya iwe vigumu kwa mtu kukubali ujumbe wa Ufalme. (Lu 18:​24-27) Ikiwa mtu anafuatilia utajiri ni vigumu kwake kukua kiroho na kukazia fikira kumpendeza Yehova.—Mt 6:24; Mk 8:36.

Onyesha VIDEO Jihadhari Usitegemee Vitu Visivyodumu!—Utajiri. Kisha waulize wasikilizaji:

8. Funzo la Biblia la Kutaniko

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 47 na Sala