2 YOHANA 1-13; 3 YOHANA 1-14–YUDA 1-25
HAZINA ZA NENO LA MUNGU |Tunapaswa Kufanya Pigano Kali Ili Kubaki Katika Kweli
Yesu alituhimiza hivi: “Jitahidini sana ili mwingie kupitia mlango mwembamba.” (Lu 13:24) Maneno ya Yesu yanaonyesha kwamba tunapaswa kupambana, kujikakamua ili tupate kibali cha Mungu. Yuda, ambaye alikuwa ndugu wa kambo wa Yesu, aliongozwa na roho kuandika maneno kama hayo: “[Fanyeni] pigano kali kwa ajili ya imani.” Tunahitaji kutia bidii ili kufanya mambo yafuatayo:
-
Kupinga kishawishi cha upotovu wa maadili kingono.—Yuda 6, 7
-
Kuwaheshimu wanaoongoza.—Yuda 8, 9
-
Kuimarisha usadikisho wetu katika ‘imani takatifu zaidi,’ yaani, mafundisho ya Kikristo.—Yuda 20, 21