Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | 2 YOHANA 1-13; 3 YOHANA 1-14YUDA 1-25

Tunapaswa Kufanya Pigano Kali Ili Kubaki Katika Kweli

Tunapaswa Kufanya Pigano Kali Ili Kubaki Katika Kweli

Yuda 3

Yesu alituhimiza hivi: “Jitahidini sana ili mwingie kupitia mlango mwembamba.” (Lu 13:24) Maneno ya Yesu yanaonyesha kwamba tunapaswa kupambana, kujikakamua ili tupate kibali cha Mungu. Yuda, ambaye alikuwa ndugu wa kambo wa Yesu, aliongozwa na roho kuandika maneno kama hayo: “[Fanyeni] pigano kali kwa ajili ya imani.” Tunahitaji kutia bidii ili kufanya mambo yafuatayo:

  • Kupinga kishawishi cha upotovu wa maadili kingono.​—Yuda 6, 7

  • Kuwaheshimu wanaoongoza.​—Yuda 8, 9

  • Kuimarisha usadikisho wetu katika ‘imani takatifu zaidi,’ yaani, mafundisho ya Kikristo.​—Yuda 20, 21