Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | UFUNUO 1-3

“Ninayajua Matendo Yako”

“Ninayajua Matendo Yako”

1:20; 2:1, 2

  • “Nyota saba”: Wazee watiwa-mafuta, na kwa maana pana zaidi, wazee wote

  • “Katika mkono [wa Yesu] wa kuume”: Yesu ana mamlaka kamili juu ya nyota hizo na anazidhibiti na kuziongoza. Ikiwa kuna mtu kwenye baraza la wazee anayehitaji kurekebishwa, Yesu atahakikisha kwamba hilo linashughulikiwa kwa wakati wake na kwa njia yake.

  • “Vinara saba vya taa vya dhahabu”: Makutaniko ya Kikristo. Kama tu kinara cha taa katika hema la ibada kilivyotoa mwangaza halisi, makutaniko ya Kikristo yanatokeza mwangaza wa kiroho. (Mt 5:14) Yesu ‘anatembea kati ya’ vile vinara vya taa katika maana ya kwamba anasimamia utendaji wa makutaniko yote