Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Yehova Anajua Mahitaji Yetu

Yehova Anajua Mahitaji Yetu

Mtumwa mwaminifu na mwenye busara hutuandalia chakula “kwa wakati unaofaa,” jambo linaloonyesha kwamba Yehova, ambaye humwongoza mtumwa huyo, anajua tunachohitaji kiroho. (Mt 24:45) Makusanyiko yetu ya eneo na mikutano yetu ya katikati ya juma ni uthibitisho unaotosha wa maandalizi hayo.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA RIPOTI YA MWAKA WA 2017 YA HALMASHAURI YA UFUNDISHAJI, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Ni nani anayepaswa kusifiwa kwa makusanyiko tunayofurahia kwa wakati unaofaa, na kwa nini?

  • Maandalizi ya kusanyiko huanza lini?

  • Habari zitakazozungumziwa kusanyikoni huchaguliwaje?

  • Ni kazi gani zinazohusika katika kuandaa makusanyiko?

  • Mbinu za kujifunza zinazotumiwa katika Shule ya Gileadi zinatumiwaje kutayarisha habari itakayotumiwa katika mkutano wa katikati ya juma?

  • Idara mbalimbali zinashirikianaje kutayarisha daftari la mkutano?

Wewe unahisije kuhusu maandalizi ya kiroho kutoka kwa Yehova?