Wapanda Farasi Wanne Katika Mwendo
Yesu ‘alienda akishinda’ kwa kupigana na Shetani na roho wake waovu mbinguni na kuwatupa duniani. Yesu anaendelea kushinda kwa niaba ya watumishi wake kwa kuwasaidia na kuwalinda katika siku hizi za mwisho. ‘Atakamilisha ushindi wake’ anapokomesha mbio za wapanda farasi wale watatu kwenye Har–Magedoni na baada ya hapo kuondoa madhara yaliyosababishwa na wapanda farasi hao.