Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Yehova Anampenda Mtoaji Mchangamfu

Yehova Anampenda Mtoaji Mchangamfu

Kwenye 2 Wakorintho 9:7, tunasoma hivi: “Kila mmoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake, si kwa kutopenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda mtoaji mchangamfu.” Leo kuna njia za kutoa michango kupitia mtandao kwa njia rahisi ili kutegemeza kazi ya Mashahidi wa Yehova katika eneo letu na pia ulimwenguni pote.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA MWONGOZO WA KUTOA MICHANGO KIELEKTRONI, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Unawezaje kupata ukurasa wa habari kuhusu michango ili kufahamu jinsi ya kutoa michango katika nchi unayoishi?

  • Baadhi ya akina ndugu na dada wamefaidikaje kwa kutoa michango kielektroni?

  • Kuna njia zipi za kutoa michango?

  • Tunaweza kufanya nini ikiwa hatuelewi jinsi ya kutumia vifaa hivi vipya vya kielektroni?