Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Desemba 23-29

ZABURI 119:​121-176

Desemba 23-29

Wimbo 31 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Jinsi ya Kuepuka Matatizo ya Kujisababishia

(Dak. 10)

Penda amri za Mungu (Zb 119:127; w18.06 17 ¶5-6)

Chukia kutenda mabaya (Zb 119:128; w93 4/15 17 ¶12)

Msikilize Yehova, na uepuke makosa ya ‘wasio na uzoefu’ (Zb 119:​130, 133; Met 22:3)

JIULIZE, ‘Ninahitaji kufanya mabadiliko gani ili nipende amri za Mungu zaidi au nichukie mabaya?’

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 119:106—Kupatana na mstari huu, tunapaswa kusadiki jambo gani? (w23.01 2 ¶2)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. (lmd somo la 1 jambo kuu la 5)

5. Kufuatia Upendezi

(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwonyeshe mwenye nyumba jinsi ya kupata habari inayompendeza kwenye jw.org. (lmd somo la 8 jambo kuu la 3)

6. Kufanya Wanafunzi

(Dak. 5) Mazungumzo pamoja na mwanafunzi wa Biblia ambaye hahudhurii mikutano ya kutaniko kwa ukawaida. (lmd somo la 12 jambo kuu la 4)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 121

7. Usiruhusu Pesa Zikusababishie Maumivu Yasiyo ya Lazima

(Dak. 15) Mazungumzo.

Wale ambao maisha yao yanaongozwa na upendo wa pesa ‘wamejichoma kila mahali kwa maumivu mengi.’ (1Ti 6:​9, 10) Hapa chini kuna baadhi ya maumivu yasiyo ya lazima ambayo tunaweza kupata ikiwa tunapenda pesa na ikiwa tunaruhusu upendo huo uongoze maisha yetu.

  • Hatutaweza kuwa na uhusiano wa karibu pamoja na Yehova.—Mt 6:24

  • Hatutawahi kutosheka.—Mhu 5:10

  • Itakuwa rahisi zaidi kushawishika kutenda mabaya, kama vile, kusema uwongo, kuiba, na kutenda kwa hila. (Met 28:20) Tukifanya makosa tutapatwa na hisia za hatia, sifa mbaya, na tutapoteza kibali cha Mungu

Soma Waebrania 13:​5, na kisha mzungumzie swali hili:

  • Ili tuepuke kupatwa na maumivu ya kihisia, tunapaswa kuwa na maoni gani kuhusu pesa, na kwa nini?

Hata ikiwa hatupendi pesa, tutapatwa na matatizo ikiwa hatuzitumii kwa hekima.

Onyesha video ya VIBONZO KWENYE UBAO Jinsi ya Kutumia Pesa Zako kwa Hekima. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Kwa nini tunapaswa kupanga bajeti, na tunaweza kuipangaje?

  • Kwa nini ni vizuri kuweka akiba fulani ya pesa?

  • Kwa nini ni jambo la hekima kuepuka madeni yasiyo ya lazima?

8. Funzo la Biblia la Kutaniko

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 101 na Sala