Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Epuka Mitego Hii Unapoongoza Funzo la Biblia

Epuka Mitego Hii Unapoongoza Funzo la Biblia

Kuzungumza Kupita Kiasi: Hupaswi kuhisi kwamba unahitaji kueleza kila kitu. Yesu alitumia maswali kuwasaidia watu wafikiri na kufikia uamuzi unaofaa. (Mt 17:24-27) Maswali yanafanya funzo liwe halisi na kukusaidia kuelewa kile ambacho mwanafunzi wako anaelewa na kuamini. (be 253 ¶3-4) Unapouliza swali, subiri mwanafunzi ajibu. Mwanafunzi anapotoa jibu lisilo sahihi, badala ya kumwambia jibu sahihi, muulize maswali ya ziada ili kumwongoza kwenye jibu sahihi. (be 238 ¶1-2) Zungumza kwa mwendo unaomruhusu mwanafunzi kuelewa mambo mapya.—be 230 ¶4.

Kufanya Habari Iwe Ngumu Kueleweka: Epuka kishawishi cha kueleza habari zote unazojua kuhusu habari unayozungumzia. (Yoh 16:12) Kazia fikira jambo kuu katika fungu. (be 226 ¶4-5) Kumweleza habari nyingi, hata ikiwa zinapendeza, kunaweza kuficha mambo makuu. (be 235 ¶3) Mara tu mwanafunzi anapoelewa jambo kuu, endelea na fungu linalofuata.

Kuzungumzia Tu Habari: Lengo letu si kumaliza habari fulani, bali ni kufikia moyo wa mwanafunzi. (Lu 24:32) Ili mwanafunzi afaidike kutokana na nguvu za Neno la Mungu, kazia maandiko ya msingi katika somo. (2Ko 10:4; Ebr 4:12; be 144 ¶1-3) Tumia mifano rahisi. (be 245 ¶2-4) Fikiria matatizo ambayo mwanafunzi anakabili na mambo anayoamini, kisha ufanye somo hilo limfae. Uliza maswali kama vile: “Unahisije kuhusiana na yale unayojifunza sasa?” “Jambo hili linatufundisha nini kumhusu Yehova?” “Unafikiri tutapata faida gani kwa kutumia ushauri huu?”—be 238 ¶3-5; 259 ¶1.