Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Watie Moyo Wanaopendezwa Wahudhurie Mikutano

Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Watie Moyo Wanaopendezwa Wahudhurie Mikutano

KWA NINI NI MUHIMU: Kuhudhuria mikutano kunatupatia nafasi ya ‘kumwimbia Yehova’ na ‘kumsifu.’ (Zb 149:1) Tunapokuwa mikutanoni, tunafundishwa kufanya mapenzi ya Mungu. (Zb 143:10) Kwa kawaida, wanafunzi wa Biblia na watu wanaopendezwa hufanya maendeleo zaidi wanapohudhuria mikutano.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Waalike mapema iwezekanavyo. Huhitaji kungoja hadi funzo la Biblia lianzishwe.—Ufu 22:17

  • Mweleze mtu anayependezwa mambo atakayoona na yatakayozungumziwa kwenye mkutano unaofuata. Vifaa vifuatavyo vinaweza kukusaidia kufanya hivyo: mwaliko wa kuhudhuria mikutano, video Ni Nini Hutendeka Katika Jumba la Ufalme?, na somo la 5 na la 7 kwenye broshua Mapenzi ya Yehova

  • Uwe tayari kumsaidia. Je, anayependezwa anahitaji usafiri au msaada wa kuchagua mavazi yanayofaa? Keti naye mkutanoni, na ushiriki naye machapisho yako. Mtambulishe kwa wengine