Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Mtoto Anapofungua Mlango

Mtoto Anapofungua Mlango

Mtoto anapofungua mlango, tunapaswa kumwomba tuzungumze na wazazi wake. Kufanya hivyo kutaonyesha tunaheshimu ukichwa wa familia hiyo. (Met 6:20) Mtoto akitukaribisha ndani, tunapaswa kukataa. Kama wazazi hawapo tunapaswa kurudi wakati mwingine.

Ikiwa mtoto huyo ana umri wa miaka 15 hivi au zaidi, bado itafaa kuomba tuongee na wazazi wake. Ikiwa hawapo, tunaweza kumwuliza ikiwa wazazi wake wanamruhusu ajichagulie habari za kusoma. Ikiwa wanamruhusu, tunaweza kumwachia machapisho na labda hata kumwelekeza kwenye Tovuti yetu ya jw.org.

Tunapomrudia kijana aliyeonyesha upendezi, tunapaswa kuomba kukutana na wazazi wake. Hivyo tutapata nafasi ya kuwaeleza kusudi la kuwatembelea na kuwaonyesha mashauri yanayoaminika na kutegemeka yanayopatikana katika Biblia kwa ajili ya familia. (Zb 119:86, 138) Kuwaonyesha wazazi heshima na ufikirio kutatoa ushahidi mzuri na huenda hilo likatupatia fursa nyingine za kushiriki habari njema na familia hiyo.—1Pe 2:12.