Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ZABURI 119

‘Tembea Katika Sheria ya Yehova’

‘Tembea Katika Sheria ya Yehova’

Kutembea katika sheria ya Yehova kunamaanisha kukubali kwa hiari mwongozo wa Mungu. Tuna mifano mingi mizuri katika Biblia ya wale ambao, kama mtunga-zaburi, walitii sheria ya Yehova na kumtegemea.

Ili tuwe na furaha ya kweli, tunahitaji kutembea katika sheria ya Mungu

119:1-8

Yoshua alionyesha kwamba alikuwa na uhakika kamili katika mwongozo wa Yehova. Alijua kwamba ili kupata furaha na mafanikio ya kweli, alihitaji kumtegemea Yehova kwa moyo wake wote

Neno la Mungu hutupa ujasiri tunaohitaji ili kukabiliana na majaribu maishani

119:33-40

Yeremia alionyesha ujasiri na alimtegemea Yehova alipokabili hali ngumu. Alidumisha maisha rahisi na alivumilia katika mgawo wake

Ujuzi sahihi wa Neno la Mungu hutupa uhakika wa kuhubiri

119:41-48

Paulo hakuogopa kuhubiri ujumbe wa Mungu kwa mtu yeyote. Alikuwa na uhakika kamili wa msaada wa Yehova alipomhubiria kwa ujasiri Gavana Feliksi

Kati ya sehemu zilizoorodheshwa, ni wapi ninaweza kuonyesha uhakika zaidi ninapowahubiria wengine?

  • Shuleni

  • Kazini

  • Katika familia

  • Nyingine