Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Oktoba 7-13

ZABURI 92-95

Oktoba 7-13

Wimbo 84 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Kumtumikia Yehova Ndiyo Njia Bora ya Maisha!

(Dak. 10)

Yehova anastahili ibada yetu (Zb 92:​1, 4; w18.04 26 ¶5)

Anawapa watu wake ufahamu usio na kifani (Zb 92:5; w18.11 20 ¶8)

Anawathamini wale wanaoendelea kumtumikia hata wanapozeeka (Zb 92:​12-15; w20.01 19 ¶18)

JIULIZE, ‘Ni nini kinachonizuia nisijiweke wakfu kwa Yehova na kubatizwa?’

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 92:5—Maneno haya yanafafanuaje hekima ya Yehova kwa njia inayofaa? (cl 176 ¶18)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Tafuta nafasi ya kumweleza mtu huyo kuhusu kazi unayofanya ukiwa mwalimu wa Biblia. (lmd somo la 5 jambo kuu la 3)

5. Kufuatia Upendezi

(Dak. 3) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Anzisha funzo la Biblia na mtu anayependezwa ambaye alikataa kujifunza wakati uliopita. (lmd somo la 8 jambo kuu la 4)

6. Kufanya Wanafunzi

(Dak. 5) Mazungumzo pamoja na mwanafunzi wa Biblia ambaye hafanyi maendeleo. (lmd somo la 12 jambo kuu la 5)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 5

7. Vijana Wanapolemewa na Mahangaiko

(Dak. 15) Mazungumzo.

Watumishi wa Yehova wanaweza kupatwa na mahangaiko. Kwa mfano, mara kwa mara Daudi alikabili mahangaiko maishani mwake, na ndivyo ilivyo kwa ndugu wengi leo. (Zb 13:2; 139:23) Kwa kusikitisha, hata vijana wanakabili mahangaiko. Nyakati nyingine, mahangaiko yanaweza kufanya utendaji wa kawaida, kama vile kwenda shuleni au kuhudhuria mikutano ya kutaniko, uonekane kuwa wenye kulemea. Huenda hata mahangaiko yakawasababishia mishtuko ya ghafla ya hofu au hata kuwafanya wawe na mawazo ya kujiua.

Vijana, wakati wowote mtakapohisi mmelemewa na mahangaiko, zungumzeni na mzazi au Mkristo mkomavu. Hakikisheni pia mnasali kwa Yehova ili kupata msaada wake. (Flp 4:6) Yeye atawasaidia. (Zb 94:​17-19; Isa 41:10) Hebu ona mfano wa Steing.

Onyesha VIDEO Yehova Alinitunza. Kisha waulize wasikilizaji:

• Ni mstari gani wa Biblia uliomsaidia Steing, na kwa nini?

• Yehova alimtunzaje?

Wazazi, mnaweza kuwasaidia watoto wenu kukabiliana na mahangaiko kwa kuwasikiliza kwa subira, kuwahakikishia kwamba mnawapenda, na kuwasaidia kuwa na uhakika kwamba Yehova anawapenda. (Tit 2:4; Yak 1:19) Mtegemee Yehova ili upate faraja na nguvu unazohitaji za kuwategemeza watoto wako.

Huenda tusijue wakati ambapo mtu kutanikoni anakabiliana na mahangaiko mazito au kuelewa jinsi anavyohisi. Hata hivyo, tunaweza kuwasaidia wote kutanikoni kujihisi wanapendwa na kuthaminiwa.—Met 12:25; Ebr 10:24.

8. Funzo la Biblia la Kutaniko

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 81 na Sala