Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Septemba 16-22

ZABURI 85-87

Septemba 16-22

Wimbo 41 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Sala Inatusaidia Kuvumilia

(Dak. 10)

Mwombe Yehova akupe shangwe (Zb 86:4)

Mwombe Yehova akusaidie uendelee kuwa mwaminifu (Zb 86:​11, 12; w12 5/15 25 ¶10)

Uwe na uhakika kwamba Yehova atajibu sala zako (Zb 86:​6, 7; w23.05 13 ¶17-18)


JIULIZE, ‘Je, mimi husali mara nyingi zaidi na kutoa sala ndefu zaidi ninapokabili majaribu?’—Zb 86:3.

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 86:11—Sala ya Daudi inadokeza nini kuhusu moyo wa mtu? (it-1 1058 ¶5)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Anzisha funzo la Biblia. (lmd somo la 3 jambo kuu la 5)

5. Kufuatia Upendezi

(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Anzisha funzo la Biblia na mtu ambaye katika mazungumzo yaliyotangulia alisema ana wasiwasi kuhusu tukio fulani la karibuni. (lmd somo la 7 jambo kuu la 4)

6. Kufanya Wanafunzi

(Dak. 5) lff somo la 15 jambo kuu la 5. Zungumzia mipango uliyofanya ya mwanafunzi wako kuendelea na funzo licha ya kwamba utasafiri juma linalofuata. (lmd somo la 10 jambo kuu la 4)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 83

7. Usife Moyo

(Dak. 5) Mazungumzo.

Onyesha VIDEO. Kisha uwaulize wasikilizaji:

  • Kwa nini wakati fulani huenda tukahisi kama tunataka kukata tamaa tunapokuwa katika huduma?

  • Kwa nini hatupaswi kufa moyo?

8. Endelea Kuanzisha Mafunzo ya Biblia!

(Dak. 10) Mazungumzo.

Je, umeanzisha funzo la Biblia kwa kutumia broshua Furahia Maisha Milele! mwezi huu wakati wa kampeni ya pekee? Ikiwa ndivyo, bila shaka hilo limekufanya uwe na shangwe sana. Huenda wengine wametiwa moyo na matokeo yako pia. Kwa upande mwingine, ikiwa bado hujaanzisha funzo la Biblia, huenda ukajiuliza ikiwa jitihada zako zina matokeo. Unaweza kufanya nini ikiwa unajihisi umevunjika moyo?

Onyesha VIDEO “Tunajipendekeza Kuwa Wahudumu wa Mungu . . . kwa Subira”—Tunapohubiri. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Andiko la 2 Wakorintho 6:​4, 6 linaweza kutusaidiaje huduma yetu inapoanza kuwa “kama shimo lisilo na mwisho”?

  • Unaweza kufanya mabadiliko gani unapohisi ni kana kwamba jitihada zako za kuanzisha funzo la Biblia hazina matokeo?

Kumbuka kwamba shangwe yetu haitegemei tunaanzisha au tunaongoza mafunzo mangapi ya Biblia. Badala yake, shangwe yetu inatokana na kujua Yehova anapendezwa na jitihada zetu. (Lu 10:​17-20) Kwa hiyo, endeleeni kushiriki katika kampeni hii ya pekee kwa moyo wote, mkijua kwamba “kazi yenu si ya bure kuhusiana na Bwana”!—1Ko 15:58.

9. Funzo la Biblia la Kutaniko

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 39 na Sala