Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Septemba 2-8

ZABURI 79-81

Septemba 2-8

Wimbo 29 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Lipende Jina Tukufu la Yehova

(Dak. 10)

Jiepushe na mazoea yanayomshushia Yehova heshima (Zb 79:9; w17.02 9 ¶5)

Liitie jina la Yehova (Zb 80:18; ijwbv 3 ¶4-5)

Yehova huwathawabisha sana wale wanaoonyesha wanalipenda jina lake kupitia utii wao (Zb 81:​13, 16)

Ili mwenendo wetu ulitukuze jina la Yehova, tunapaswa kujitambulisha kuwa Mashahidi wake

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 80:1—Kwa nini pindi fulani jina la Yosefu lilitumiwa kuwakilisha makabila yote ya Israeli? (it-2 111)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 1) NYUMBA KWA NYUMBA. Anzisha funzo la Biblia. (lmd somo la 4 jambo kuu la 4)

5. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Anzisha funzo la Biblia. (lmd somo la 4 jambo kuu la 3)

6. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 2) MAHUBIRI YA UMMA. Anzisha funzo la Biblia. (lmd somo la 3 jambo kuu la 3)

7. Kufuatia Upendezi

(Dak. 5) NYUMBA KWA NYUMBA. Anzisha funzo la Biblia na mtu anayependezwa ambaye alikataa kujifunza wakati uliopita. (lmd somo la 8 jambo kuu la 3)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 10

8. “Watalitakasa Jina Langu”

(Dak. 15) Mazungumzo.

Kwenye bustani ya Edeni Shetani alianza kumchongea Yehova na hivyo kulichafua jina lake. Tangu wakati huo, suala muhimu zaidi linalowakabili viumbe wote wenye akili ni kutetewa kwa jina la Yehova.

Fikiria baadhi ya uwongo mbaya ambao Shetani ameeneza kumhusu Yehova. Amemshtaki kuwa mtawala mkatili ambaye hana upendo. (Mwa 3:​1-6; Ayu 4:​18, 19) Anadai kwamba waabudu wa Yehova hawampendi kikweli. (Ayu 2:​4, 5) Hata amewafanya mamilioni ya watu waamini kwamba Yehova si Muumba wa ulimwengu wetu maridadi.—Ro 1:​20, 21.

Wewe unahisije kuhusu uwongo huo? Huenda unahisi kwamba ungependa kumtetea Yehova! Alijua kwamba watu wake wangetamani kusaidia kulitakasa jina lake. (Linganisha Isaya 29:23.) Wewe unaweza kusaidiaje?

  • Wasaidie wengine wamjue na kumpenda Yehova. (Yoh 17:​25, 26) Uwe tayari kuwathibitishia wengine kwamba yeye yupo na kuwafundisha kuhusu sifa zake zenye kustaajabisha.—Isa 63:7

  • Mpende Yehova kwa moyo wako wote. (Mt 22:​37, 38) Tii amri za Yehova—si kwa sababu tu utafaidika—bali kwa sababu unataka kumfurahisha Yehova.—Met 27:11

Onyesha VIDEO Upendo Haushindwi Kamwe Licha ya . . . Watu Wasiomwogopa Mungu Shuleni. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Ariel na Diego waliteteaje jina la Yehova?

  • Ni nini kilichowachochea kuchukua msimamo upande wa Yehova?

  • Unaweza kuigaje mfano wao?

9. Funzo la Biblia la Kutaniko

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 90 na Sala