Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Yehova Huwaokoa Waliopondeka Roho

Yehova Huwaokoa Waliopondeka Roho

Kila mtu huhuzunika mara kwa mara. Kuwa na huzuni hakumaanishi mtu ni dhaifu kiroho. Kwa kweli, Yehova mwenyewe alifunua kwamba pindi fulani anahuzunika. (Mwa 6:​5, 6) Lakini vipi ikiwa tunahisi tumelemewa na huzuni mara nyingi au wakati wote?

Mwombe Yehova msaada. Yehova anapendezwa sana na afya yako ya kiakili na ya kihisia. Anajua wakati ambapo tuna furaha na wakati ambapo tumehuzunika. Anaelewa sababu zinazotufanya tuhisi au kufikiri kwa njia fulani. (Zb 7:9b) Jambo muhimu hata zaidi, Yehova anatujali na anaweza kutusaidia kukabiliana na hisia za huzuni au hata za kushuka moyo.—Zb 34:18.

Tunza afya yako ya akili. Hisia zisizofaa zinaweza kutunyima shangwe na kuathiri ibada yetu. Kwa sababu hiyo, tunapaswa kulinda moyo wetu—yule mtu tuliye kwa ndani.—Met 4:23.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA JINSI NDUGU ZETU WANAVYOFURAHIA AMANI LICHA YA KUSHUKA MOYO, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Nikki alifanya mambo gani yanayofaa ambayo yalimsaidia kukabiliana na kushuka moyo?

  • Kwa nini Nikki alihisi kwamba alihitaji kutafuta matibabu?—Mt 9:12

  • Nikki alitegemea msaada wa Yehova katika njia zipi?