Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Wazazi—Wasaidieni Watoto Wenu Kupata Hekima Kutoka kwa Mungu

Wazazi—Wasaidieni Watoto Wenu Kupata Hekima Kutoka kwa Mungu

Njia moja muhimu ambayo wazazi wanaweza kuwasaidia watoto wao kupata hekima kutoka kwa Mungu ni kwa kuwasaidia kunufaika kutokana na mikutano. Mambo ambayo watoto wanaona, kusikia, na kusema wanapotoa maelezo mikutanoni yanaweza kuwasaidia kujifunza kumhusu Yehova na kuwa rafiki yake wa karibu. (Kum 31:​12, 13) Ikiwa wewe ni mzazi, unaweza kumsaidiaje mtoto wako kunufaika kikamili kutokana na mikutano?

  • Fanya yote uwezayo kuhudhuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme.—Zb 22:22

  • Hakikisha kwamba unakuwa na muda wa kutiana moyo na ndugu na dada kwenye Jumba la Ufalme kabla au baada ya mikutano.—Ebr 10:25

  • Hakikisha kila mshiriki wa familia ana nakala ya machapisho yatakayotumiwa kwenye mikutano, iwe ni ya kielektroni au yaliyochapishwa

  • Msaidie mtoto wako atayarishe maelezo kwa maneno yake mwenyewe.—Mt 21:​15, 16

  • Zungumza kwa njia inayofaa kuhusu mikutano na mambo tunayojifunza mikutanoni

  • Wasaidie watoto wako wajihusishe katika utendaji kama vile kufanya usafi kwenye Jumba la Ufalme na kuzungumza na watu wenye umri mkubwa kutanikoni

Kuwasaidia watoto kumkaribia Yehova kunahitaji jitihada nyingi, na huenda wakati mwingine ukahisi umelemewa. Hata hivyo, unaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atakusaidia.—Isa 40:29.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA WAZAZI—MTEGEMEENI YEHOVA ILI AWAPE NGUVU, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Zack na Leah walikuwa wakiathiriwaje na uchovu?

  • Kwa nini wazazi wanapaswa kumwomba Yehova awape nguvu?

  • Zack na Leah walimtegemea Yehova katika njia zipi ili wafanikiwe?