Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kwa Nini Hakuna Heshima Katika Familia?

Kwa Nini Hakuna Heshima Katika Familia?

KWA NINI NI MUHIMU KUWA NA HESHIMA KATIKA FAMILIA

Familia inakuwa na amani washiriki wake wanapoheshimiana.

  • Kitabu The Seven Principles for Making Marriage Work kinasema kwamba wenzi wa ndoa wanapoheshimiana, wanaonyeshana upendo “si katika mambo makubwa tu bali pia katika mambo madogo-madogo kila siku.”

  • Utafiti unaonyesha kwamba watoto wanaofundishwa kuwaheshimu wengine hujiamini, hufurahia uhusiano mzuri zaidi na wazazi wao, na hawana matatizo mengi ya kihisia.

JAMBO UNALOWEZA KUFANYA

Fanyeni mipango mkiwa familia. Kwanza, hakikisha kwamba kila mtu katika familia anaelewa jinsi ya kuonyesha heshima. Pili, andikeni mambo ambayo kila mtu katika familia anapaswa kufanya na mambo ambayo anapaswa kuepuka. Tatu, mkiwa familia, fanyeni mipango na mzungumzie kile ambacho ninyi na watoto wenu mnapaswa kufanya ili kuonyeshana heshima.

“Mipango ya wenye bidii hakika huleta mafanikio.”—Methali 21:5.

Weka mfano mzuri. Je, wewe huwachambua watu wa familia yako kwa sababu ya makosa yao, unawakejeli kwa sababu ya maoni yao, au unawapuuza au kukatiza mazungumzo wanapoongea na wewe?

Dokezo: Ona heshima kuwa jambo ambalo unapaswa kumwonyesha mwenzi wako na watoto wako, na si jambo ambalo wanahitaji kufanyia kazi ili wastahili kupata.

“Katika kuonyeshana heshima, iweni wa kwanza.”—Waroma 12:10.

Waonyeshe wengine heshima hata kama hukubaliani na maoni yao. Unapojieleza, epuka kutumia maneno kama “ni kawaida yako” au “haujawahi.” Maneno kama hayo yatamuumiza sana mshiriki wa familia yako na yatasababisha tatizo dogo liwe kubwa.

“Jibu la upole hutuliza hasira, lakini neno kali huchochea hasira.”—Methali 15:1.

MAMBO TUNAYOFANYA

Mashahidi wa Yehova huwatia moyo washiriki wa familia watendeane kwa heshima, wakifanya hivyo mara nyingi kupitia makala, vitabu, broshua, na video wanazotoa bila malipo.

KWA AJILI YA WENZI WA NDOA: Mfululizo wa makala Msaada kwa Ajili ya Familia unaweza kuwasaidia waume na wake kuwa . . .

  • wasilikilizaji wazuri

  • kukomesha tabia ya kunyamaziana

  • kuacha kugombana

(Tafuta “Msaada kwa Ajili ya Familia” kwenye jw.org/sw)

KWA AJILI YA WAZAZI: Mfululizo wa makala Msaada kwa Ajili ya Familia unaweza kuwasaidia wazazi kuwazoeza watoto wao . . .

  • wawe watiifu

  • wasaidie kazi za nyumbani

  • waseme “tafadhali” na “asante”

(Tafuta “Kulea Watoto” na “Kulea Matineja” kwenye jw.org/sw)

Ona pia nyongeza, “Maswali Ambayo Wazazi Huuliza,” kwenye kitabu Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1. (Tafuta “Maswali Ambayo Wazazi Huuliza” kwenye jw.org/sw)

KWA AJILI YA VIJANA: Sehemu ya Matineja kwenye jw.org ina makala, video, na daftari ambazo zinaweza kuwasaidia vijana . . .

  • kupatana na wazazi wao na ndugu zao

  • kuzungumza na wazazi wao kwa heshima kuhusu sheria walizoweka

  • kuaminiwa na wazazi wao

(Tafuta “Matineja” kwenye jw.org/sw)

Unaweza kutumia tovuti ya jw.org bila malipo. Hautahitaji kujisajili, kutoa ada, au kulipia gharama, na hautaombwa kutoa taarifa zako za kibinafsi.