Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Utangulizi

Utangulizi

Siri 12 za Familia Ambazo Zimefanikiwa

Mara nyingi tunasikia kuhusu kile kinachosababisha familia fulani ziwe na matatizo. Hata hivyo, ni nini kinachoziwezesha familia nyingine kufaulu?

  • Kati ya mwaka 1990 na 2015, kiwango cha talaka nchini Marekani kiliongezeka mara mbili kwa wenzi wa ndoa walio na umri wa miaka zaidi ya 50 na mara tatu kwa wale walio na miaka zaidi ya 65.

  • Wazazi wako njia panda: Baadhi ya wataalamu wanapendekeza kwamba inafaa watoto wasifiwe kila wakati, ilhali wengine wanasema kwamba watoto hawapaswi kudekezwa hata kidogo.

  • Vijana wanaingia utu uzima bila kuwa na sifa wanazohitaji ili wafanikiwe maishani.

Ingawa hivyo, ukweli ni kwamba . . .

  • Inawezekana kabisa ndoa ikadumu na kuwa yenye furaha.

  • Wazazi wanaweza kujifunza kuwatia nidhamu watoto wao kwa upendo.

  • Vijana wanaweza kusitawisha sifa watakazohitaji wakiwa watu wazima.

Jinsi gani? Toleo hili la Amkeni! litazungumzia siri 12 zinazoziwezesha familia kufanikiwa.