Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Jambo Lililoonwa

Jambo Lililoonwa

Kuwahurumia Watu Wote

Siku moja, dada nchini New Zealand alitazama video yenye kichwa ‘Mtunzane,’ inayozungumzia jinsi Yehova anavyohisi huruma na pia anavyoionyesha. (Isa. 63:​7-9) Aliamua kutumia mambo aliyojifunza kwa kutoa msaada unaofaa. Siku hiyohiyo jioni alipoenda kununua mahitaji ya nyumbani, alikutana na mwanamke asiye na makao na akaamua kumnunulia mwanamke huyo chakula. Mwanamke huyo alikubali. Dada huyo alipomletea chakula, alimtolea ushahidi mwanamke huyo kwa kutumia trakti Je, Kuteseka Kutaisha?

Mwanamke huyo alianza kulia. Alieleza kwamba alilelewa katika familia ya Mashahidi lakini aliacha kweli miaka mingi iliyopita. Hivi karibuni, amekuwa akisali kwa Yehova akimwomba amsaidie kumrudia. Dada alimpa mwanamke huyo Biblia na kufanya mipango ya kujifunza naye Biblia. a

Kama Yehova, tunaweza kuwaonyesha watu huruma, kutia ndani watu wetu wa ukoo na ndugu na dada zetu kutanikoni. Na tunaweza kuonyesha huruma kwa kutafuta nafasi za kuwatolea wengine ushahidi.

a Ili ujifunze jinsi ya kuwasaidia wasiotenda, tazama makala yenye kichwa “Nirudieni” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 2020.