Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umesoma kwa makini matoleo ya Mnara wa Mlinzi ya mwaka huu? Ona ikiwa unaweza kujibu maswali yafuatayo:

‘Kufanya upya akili yetu’ kunahusisha nini? (Rom. 12:2)

Kunahusisha mengi zaidi ya kufanya matendo mengi mema maishani mwetu. Kunatia ndani kujichunguza jinsi tulivyo moyoni na kufanya mabadiliko ili kuyapatanisha kabisa maisha yetu na viwango vya Mungu.—w23.01, uku. 8-9.

Tunawezaje kuonyesha usawaziko tunapotazama matukio ya ulimwengu?

Tunapendezwa tunapoona jinsi matukio ya sasa yanavyotimiza unabii wa Biblia. Badala ya kukisia mambo, jambo ambalo linaweza kuvuruga umoja wetu, ni vema ikiwa msingi wa mazungumzo yetu ni habari zilizochapishwa na tengenezo la Yehova. (1 Kor. 1:10)—w23.02, uku. 16.

Ubatizo wa Yesu unatofautianaje na ubatizo wa wafuasi wake?

Tofauti na sisi, Yesu hakuhitaji kujiweka wakfu kwa Yehova, kwa sababu alizaliwa katika taifa lililowekwa wakfu kwa Mungu. Yesu alikuwa mwanadamu mkamilifu, asiye na dhambi. Hakuhitaji kutubu dhambi.—w23.03, uku. 5.

Tunaweza kuwasaidiaje wengine watoe maelezo mkutanoni?

Tunaweza kutoa maelezo mafupi ili kuwaruhusu wengine washiriki. Pia, tunaweza kuepuka kuzungumzia mambo mengi sana. Hivyo, wengine watapata jambo la kusema.—w23.04, uku. 23.

“Njia ya Utakatifu” inayotajwa kwenye Isaya 35:8 inarejelea nini?

Mwanzoni, ilirejelea barabara ya mfano iliyotoka Babiloni kwenda kwenye nchi ya Wayahudi. Namna gani katika nyakati za karibuni zaidi? Karne nyingi kabla ya mwaka wa 1919, kazi ya kutayarisha barabara hiyo kuu ilifanywa—mojawapo ya mambo yaliyofanywa ni kutafsiriwa na kuchapishwa kwa Biblia. Watu wa Mungu wamekuwa wakisafiri kwenye “Njia ya Utakatifu” kuelekea kwenye paradiso ya kiroho inayoongoza kwenye baraka za Ufalme.—w23.05, uku. 15-19.

Methali sura ya 9 inatoa ushauri gani unaotegemea wanawake wawili wa mfano?

Sura hiyo katika kitabu cha Methali inamzungumzia “mwanamke mpumbavu” ambaye mwaliko wake unaongoza kwenye “Kaburi” na pia “hekima ya kweli” inalinganishwa na mwanamke ambaye mwaliko wake unaongoza kwenye “njia ya uelewaji” na uzima. (Met. 9:​1, 6, 13, 18)—w23.06, uku. 22-24.

Mungu alionyeshaje unyenyekevu na usawaziko aliposhughulika na Loti?

Yehova alimwagiza Loti atoke Sodoma na akimbilie kwenye eneo lenye milima. Loti alipomsihi Mungu akimbilie eneo tofauti la Soari, alikubali ombi lake.—w23.07, uku. 21.

Mke anaweza kufanya nini ikiwa mwenzi wake anatazama ponografia?

Mke anapaswa kukumbuka kwamba hana lawama yoyote. Anapaswa kukazia uangalifu uhusiano wake na Mungu na kutafakari masimulizi ya Biblia kuhusu wanawake waliopata matatizo ambao walifarijiwa na Mungu. Anaweza kumsaidia mume wake aepuke hali zinazoweza kumshawishi.—w23.08, uku. 14-17.

Ufahamu unawezaje kutusaidia kuwa wapole wengine wanapopinga imani yetu?

Tunaweza kuona swali au jambo analopinga kuwa njia ya kutambua mambo ambayo mtu anafikiria au anayaona kuwa muhimu. Hivyo, tutakuwa tayari zaidi kujibu kwa njia ya upole.—w23.09, uku. 17.

Tunaweza kujifunza nini kutoka kwa Maria kuhusu kupata nguvu?

Alipotambua kwamba angekuwa mama wa Masihi, Maria alipata nguvu kutoka kwa wengine. Gabrieli na Elisabeti walimtia moyo Maria kwa kutumia Maandiko. Sisi pia tunaweza kutiwa nguvu na waabudu wenzetu.—w23.10, uku. 15.

Yehova anaweza kujibuje sala zetu?

Anaahidi kusikiliza sala zetu na anazingatia jinsi zinavyohusiana na kusudi lake. (Yer. 29:12) Huenda akajibu maombi yanayofanana kwa njia mbalimbali, lakini sikuzote atatutegemeza.—w23.11, uku. 21-22.

Waroma 5:2 inataja “tumaini,” basi kwa nini linazungumziwa tena kwenye mstari wa 4?

Mtu anaweza kupata tumaini la kufurahia maisha katika paradiso duniani anaposikia habari njema. Lakini anapokabili majaribu, anapoyavumilia, na kuhisi ana kibali cha Mungu, inaelekea tumaini lake litakuwa imara na kuwa halisi zaidi kwake.—w23.12, uku. 12-13.