Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Magazeti Bora Zaidi Yawezayo Kupatikana”

“Magazeti Bora Zaidi Yawezayo Kupatikana”

“Magazeti Bora Zaidi Yawezayo Kupatikana”

HIVI KARIBUNI wahariri wa gazeti Amkeni! walipokea barua kutoka kwa Lisel, mwanafunzi wa shule ya sekondari mwenye umri wa miaka 18 huko Marekani. Aliandika hivi:

“Nimejiandikisha katika mtalaa wa somo la Historia katika chuo. Kuna mtihani unaohusisha utafiti mwingi, nami nimechagua kuandika kuhusu jinsi Mashahidi wa Yehova walivyoshikilia maadili yao wakati wa Utawala wa Nazi huko Ujerumani. Ningependa kuomba orodha ya marejezo yaliyotolewa mwishoni mwa makala ya Amkeni! iliyokuwa na kichwa ‘Mashahidi wa Yehova—Wajasiri Licha ya Hatari ya Wanazi’ ambayo ilikuwa kwenye toleo la Julai 8, 1998. Makala hiyo ilifanyiwa utafiti kikamili na iliandikwa kwa mantiki hivi kwamba nikiandika mtihani wangu kwa kutumia nusu tu ya mawazo na kweli mlizotoa, matokeo yatakuwa ushahidi mkubwa kwa wale watakaosahihisha kazi yangu.

“Asanteni kwa kuendelea kutokeza magazeti bora zaidi yawezayo kupatikana. Katika kila toleo, ninapata ‘masomo niwezayo kuandika juu yake’ bora zaidi kuliko yoyote yanayotolewa katika shule yangu, na jambo hili hunichochea kutaka kufanya vema zaidi katika kila mtihani nifanyao. Tafadhalini jueni kwamba nathamini jitihada zenu.”

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 22]

Picha iliyo katikati: Państwowe Muzeum Oświęcim-Brzezinka, courtesy of the USHMM Photo Archives